MZEE MKAPA NA MZEE KIKWETE WAACHWA WAPUMZIKE– RAIS MAGULI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli
amevionya vyombo vya habari vinavyowachafua Marais wastaafu, Benjamin
Mkapa na Jakaya Kikwete huku akivitaka viwaache wapumzike.
![](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_uPdKIm2dAWIb7Ksn1F6vftafresjPITp5YYn2WcDLY34mCTNyDhcIeHYggSlN_51CyyfjstXb-ObTpodXsSu7G-ewSYjVcb72mJb4dZC_SWSTnohNeftk=s0-d)
Rais Magufuli ameyasema hayo leo ,Ikulu jijini Dar es salaam baada ya kukutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Barrick ya nchini Canada, Profesa John Thornton walipokutana kuzungumzia sakata la Makinikia.
“Nimesoma ripoti zote mbili hakuna mahali ambapo Mzee Mkapa na Mzee Kikwete wametajwa, vyombo vya habari viache kuwachafua hawa wazee, wamefanya kazi kubwa ya kulitumikia Taifa letu, viwaache wapumzike,” amesema Rais.
Rais Magufuli ameyasema hayo leo ,Ikulu jijini Dar es salaam baada ya kukutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Barrick ya nchini Canada, Profesa John Thornton walipokutana kuzungumzia sakata la Makinikia.
“Nimesoma ripoti zote mbili hakuna mahali ambapo Mzee Mkapa na Mzee Kikwete wametajwa, vyombo vya habari viache kuwachafua hawa wazee, wamefanya kazi kubwa ya kulitumikia Taifa letu, viwaache wapumzike,” amesema Rais.
No comments: