Bnner

Breaking News
recent

BONGO MOVIE HAWANA UHALISI – MCH ANTHONY LUSEKELO



Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo alimaarufu kama ‘Mzee wa Upako’ anashangaa Waigizaji wa Bongo Movie kwa kuigiza vitu ambavyo havina uhalisia kama filamu za wenzetu walioendelea.

Tokeo la picha la mzee wa upako
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo
Mzee wa Upako amesema anawashangaa Waigizaji hao kuandamana kwa kudai wanaharibiwa soko na filamu za kigeni ile hali vitu wanavyoigiza havina uhalisia kabisa kwenye jamii yetu kwani utakuta mtu anaigiza kama Meneja wa kampuni kubwa lakini utakuta kavaa hereni na nywele kaweka dawa.

Vijana wa Bongo Movie wanalalamika kuwa hawana soko lakini soko wameharibu wenyewe… utakuta mtu katika sinema moja anaanza kuwa shemeji wa mtu fulani inaisha anakuwa kaka sasa hawa jamaa mimi….mhhhhh !!”amesema Mzee wa Upako huku akiendelea kuhoji kwa mshangao

Hata hivyo Mchungaji Lusekelo hakuishia Bongo Movie tuu amewashauri pia Wasanii wa muziki wa injili kuwa wamoja kama walivyo Wasanii wa Bongo Fleva kwa kufanya kolabo nyingi.

No comments:

Powered by Blogger.