MABAKI YA BINADAMU WA KWANZA YALIPATIKANA MOROCCO
Uchunguzi umebainisha kuwa dhana ya
kuwa asili ya binadamu wa kwanza ni kutoka Afrika ya Mashariki zaidi ya
miaka laki mbili iliyopita sio kweli.
Prof Jean-Jacques Hublin, kutoka Leipzig, Ujerumani, anasema kuwa ugunduzi huu unaweza "kuandika upya vitabu vya kiada" kuhusu kuibuka kwetu .
"Sio hadithi ya hayo kutokea kwa njia ya haraka katika 'shamba la Edeni' mahali fulani barani Afrika. Ilikuwa ni maendeleo ya taratibu. Kwa hiyo kama kulikuwa na bustani ya Edeni, ilikuwa ni kote kote Afrika.
Mabaki hii ya sasa inadaiwa kuwa na umri wa kati ya miaka 300,000 na 350,000 miaka. Na fuvu yake ni ya aina karibu sawa na ya binadamu wa kisasa.
Hadi sasa, mabaki ya binadamu wa kwanza yalikuwa kutoka Ethiopia (kutoka tovuti inayojulikana kama Omo Kibish) , Afrika mashariki na walidaiwa kuwa na umri wa takribani miaka 195,000.
Kabla ya watu wa aina yetu, kulikuwa na aina nyingi tofauti ya binadamu, na kila alikuwa na uwezo na udhaifu tofauti. Na hawa aina mbalimbali ya binadamu, kama vile wanyama wengine, waliendelea kubadili muonekano wao hatua kwa hatua.
Jebel Irhoud inafanana na sehemu kadhaa za kihistoria barani Afrika ambayo ina miaka 300,000. Maeneohaya yana zana sawa na pia ushahidi wa matumizi ya moto.
No comments: